UUNDAJI WA MANENO
Uundaji wa maneno ni ujenzi au uzalishaji au utengenezaji wa maneno mapya. Uundaji wa maneno mapya husaidia kuongeza msamiati katika lugha ili kukidhi mahitaji ya mawasiliano. Uundaji wa maneno mapya husababishwa na mabadiliko ya kiuchumi, kisiasa na kiutamaduni na maendeleo ya kisayansi yanayotokea katika jamii. Kwa mfano tunayo maneno mapya, kama vile ufisadi, uwekezaji, ukeketaji, ujasiriamali na mengine mengi kutokana na mabadiliko ya kijamii.
Kubainisha Mofimu katika Maneno
Bainisha mofimu katika maneno
Uambishaji wa maneno ni kitendo cha kupata maneno kwa kubandika Mofimu kwenye kiini cha neno, uambishaji kutokea kabla ya kiini cha neno au mzizi wa neno. Mfano kiini pig- unaweza kuunda maneno kama inapiga, anayepiga, mpigaji, amepigika nk.
Mofimu zinazobadilika kwenye kiini cha neno huitwa Viambishi.
Katika lugha ya Kiswahili viambishi hutokea kabla na baada ya kiini cha neno.
Mfano
Wanapendana = Wa-na-pendan-a kiini cha neno ni-pend-.
Mofimu zilizobadilisha baada ya kiini –an-na-a viambishi vinavyotokea kabla ya kiini cha neno huitwa viambisha awali au tangulizi. Viambisha vinavyotokea baada ya kiini cha neno huitwa viambishi tamati au fuatishi.
Example 1
Angalia mifano ifuatayo:
NenoViambisha AwaliKiiniViambisha Tamati
Unapendeleau-na--penda-el-e-a
Waliongozanawa-li--ongoz-an-a
Analimaa-na--lim--a
anayeiimbishaa-na-ye-imb--ish-a
Dhima za Mofimu
Bainisha dhima za mofimu
Baadhi ya dhima za uambishaji ni kama ifuatavyo:
  1. Kuonyesha upatanisho wa usanifu maana ya maneno yanayozalishwa kutofautiana katika msingi wa kusanifu tu, lakini uhusiano wa maneno hayo hutokana na kiini au mzizi wake uleule.Mfano;Fundisha kiini chake ni fund. Unaweza kuzalisha maneno mengine kwa kutumia mzizi/kiini kilichopo kama vile fundishana, mafundisho, mfundishaji, fundishwa, fundishana.
  2. Uambishaji huonyesha nafsi
  3. Uambashaji huonyesha njeo (muda)
  4. Uambishaji huonyesha urejeshi
  5. Uambishaji huonyesha ukanushi
  6. Uambishaji huonyesha hali mbalimbali za kitenzi
Vitenzi vikiambishwa huweza kujenga/kuunda/kuzalisha vitenzi vingine au nomino.
Example 2
Mfano
VitenziKiiniNominoVitenzi
Cheza-chez-Mchezaji, mchezowanacheza/atamchezea
Piga-pig-Mpigaji, Mpiganajiwatanipiga, aliyempiga/wanaompiga
Uambishaji hutumika kuzalisha viwakilishi na vielezi.
Neno (Kiwakilishi)KiiniKielezi
Huyu, HuyoHuHumu, humo
Wangu, wako, wakewa
Hii, hizo, hikihi
Viambishi awali vina dhima ya kudokeza nafsi, njia, idadi urejeshi na ukanushi.Mfano: Hawakulima
  • Ha-, kiambishi cha ukanushi
  • Ku-, kiambishi njeo/wakati
Viambishi tamati vina dhima mbalimbali hudokeza hali ya utendekaji, ukamilishaji au kimalizio cha neno na kauli za matendo kama vile kutendwa, kutendewa,kutendeka nk.
Dhima:Ukanusho, kutendeana, agizo na mtendwa, ukamilisho, usababishi.
Example 3
Mfano
NenoViambishi Tamati
Anapiga-a
Wanapigana-an
Asipigwe-w
Amempigisha-ish-
Viambishi tamati vina dhima ya kutambulishwa mapema/nomino zilizoundwa kutokana na vitenzi.
NenoKiiniViambishi Tamati
Pigapig--o
Mchezochez--o
Mtembezitembe--z-i
Mfiwa-fi--us-a


Mazingira yanayosababisha Mahitaji ya Maneno Mapya
Elezea mazingira yanayosababisha mahitaji ya maneno mapya
Mnyumbulisho ni neno linalotokana na neno nyumbua. Kunyumbua kitu ni kuvuta, kuongeza urefu wa kitu hicho.
Kunyumbua katika lugha ya Kiswahili ni kuongeza vinyumbulishi katika katika kiini ili kupata msamiati mpya. Hivyo basi, mnyumbulisho ni njia mojawapo na inasaidia kuunda maneno kwa njia ya kunyumbulisha.
Viambishi vinapochukuliwa katika kiini cha neno, basi neno hilo huwa limenyumbulishwa. Kwa mfano neno lima kiini chake lim- huweza kunyumbulishwa na kupata maneno mengine mpya, kama lim-ishwa, lim-ia, lim-w-a.
Pia maneno ya mnyumbulisho yanaweza kuundwa kwa kuongeza viambishi kwenye shina, kwa mfano:
NenoKiiniShinaManeno ya Mnyumbuliko
ElekeaelekelekaElekeana, elekea, elekwa, elekesha
ShikishanashikshikishaShikishana, shikisha, shikishaneni
Kwa ujumla tunawaza kusema kuwa maneno ya kawaida hunyumbulika. Hivyo kiini/mzizi au shina moja huweza kuzalisha maneno mengine mengi ambayo yanatokana na msingi mmoja wa maana.
Dhima ya Uambishaji na Mnyambulikoa wa Maneno
Fafanua dhima ya uambishaji na mnyambulikoa wa maneno
Dhima ya uambishaji ni kuleta upatanisho wa kisarufi, kuonesha idadi na umoja na wingi katika ngeli za majina, kuonesha njeo na kuonesha urejeshi pamoja na hali mbalimbali kwa uambikaji wa viambishi kabla ya mzizi wa neno. Aidha dhima ya mnyambuliko ni kuonesha matokeo ya tendo na kuzalisha kauli mbalimbali kwa kupachika viambishi baada ya mzizi wa neno.
Kuunda Maneno mbalimbali kwa kutumia Mnyambuliko
Unda maneno mbalimbali kwa kutumia mnyambuliko
Uundaji wa maneno mbalimbali kwa kutumia mnyambuliko hufanyika kwa kupachika viambishi baada ya mzizi wa neno na hivyo kulifanya neno husika liweze kuonesha matokeo mbalimbali ya matendo pamoja na kuzalisha kauli mbalimbali za matendo.
Activity 1
Unda maneno mbalimbali kwa kutumia mnyambuliko
Kutumia Maneno ya Mnyambuliko katika Miktadha mablimbali
Tumia maneno ya mnyambuliko katika miktadha mablimbali
Maneno ya mnyambuliko hutumika katika miktadha mbalimbali ambapo miktadha hiyo hujitokeza katika kauli mbalimbali za vitenzi. Kauli hizo ni kauli ya kutenda, kauli ya kutendwa, kauli ya kutendewa, kauli ya kutendea, kauli ya kutendeka, kauli ya kutendesha, kauli ya kutendana, na kauli ya kutendama.
Activity 2
Tumia maneno ya mnyambuliko katika miktadha mbalimbali

logoblog

No comments:

Post a Comment