Thursday, April 13, 2023

FORM TWO CHEMBA KISWAHILI MOCK EXAMINATIONS WITH ANSWERS | MTIHANI NA MAJIBU (MARKING SCHEME) YA MTIHANI WA MOCK KISWAHILI WILAYA YA CHEMBA

  Eli-express       Thursday, April 13, 2023

JAMHURI YA MUUNGANO WA TANZANIA

 

OFISI YA RAIS TAMISEMI

MKOA WA  DODOMA

MTIHANI WA UTAMILIFU (MOCK) KIDATO  CHA PILI -2021

021 KISWAHILI

 

MUDA SAA 2: 30

 

MAAGIZO

·       Mtihani  huu una sehemu AB,C,D NA E

·       Jibu maswali yote 

 

KWA MATUMIZI YA WATAHINIWA TU


www.onlineschoobase.com

 

NAMBA YA

SWALI

ALAMA

 

 

SAINI

01

 

 

 

 

02

 

 

 

 

03

 

 

 

 

04

 

 

 

 

05

 

 

 

 

TOTAL

 

 

 

 

 

UFAHAMU A: (ALAMA (15)

1. Soma habari ifuatayo kisha jibu maswali yafuatayo 

  Dalali  alianza kumnadi beberu akisema ,haya leo  tena jamani sogeeni mjipatie vitu bei  nafuu .Oneni  mnyama mnono huyu ,shilingi  elfu sita  na mia tano .Nani atakaye na atalipa shilingi ngapi ? Mzabuni wa kwanza  alipandisha bei hadi shilingi  elifu saba na miambili  .Toka hapo bei ilizidi kupanda vikali  ajabu  , hatimaye mzabuni wa mwisho alikubali kutoa elfu kumi .

 

MASWALI

a)     Dalali alitaja bei gani kama  kianzio cha bei ya beberu

b)     Mzabuni  wa  kwanza alitaka kulipa shilingi ngapi?

c)     Eleza haya     tena jamani sogeeni .Ina maana gani ?

d)     Eleza maana ya maneno yafuatayo -:

(1) dalali

     (ii)Zabuni

(iii) Nafuu

e)     Andika kichwa cha habari hii

 

SEHEMU B (ALAMA 15) UTUMIZI WA LUGHA NA USAHIHI WA MAANDISHI

 

2 (a). Kwa kuzingatia matumizi ya Kiswahili sanifu sentensi zifuatazo zinamakosa. Ziandike upya kwa  ufasaha

MFANO . Kiti mkubwa amevunjika

 kiti kikubwa kimevujika

(i) Chai imeingia Inzi

(ii) anakwenda baba  kesho safari

(iii) Humwambiaga lakini hanielewi

(iv) Ng’ombe zangu zimeibiwa

(v) Daktari nina kifua sijalala usiku kucha

(b)  Kama lugha isingekuwepo katika jamii ya binadamu unafikiri ni matatizo gani manne ambayo yangetokea

(c) Oanisha orodha A na  B  ili kujenga  dhana sahihi. Onyesha majibu yako kwa kisanduku kama hiki

 

ORODHA A

i

ii

iii

iv

v

ORODHA B

 

 

 

 

 

 

ORODHA A 

(i) huonyesha mpangilio wa maneno kialifabeti jinsi yanavyoandikwa kutamkwa na maana zake

(ii) Lugha  ya mazungumzo  na lugha ya maandishi 

iii)Maneno yasiyo sanifu yanayozungumza na kikundi kidogo cha watu

(iv)  Taaluma inayoshughulikia maumbo au mjengo wa maneno katika tungo

(v) Ni  Mtindo wa lugha inayozungumzwa kulingana na muktadha na kusudi maalumu

 

ORODHA B

A- Tanzu za lugha

B. Rejesta

C- simo

D. Sarufi maumbo

E. Misemo

F. Mofimu

G. Nomino

H. Kamusi      

 

 

 

 

 

 

 

 

 

SEHEMU C. ALAMA 15

SARUFI

3. Bainisha aina ya maneno yaliyopigiwa mstari kwenye tungo zifuatazo kwa kuandika kifupisho cha aina ya maneno kilicho sahihi (T,t, E,V,W,H,U)

 

        i.          Ngo’ombe huyu ana  matata sana

      ii.          Kitanda cha kwanza kushoto ndicho alichotandika

    iii.          Macho yake malegevu

     iv.          Yule mchezaji aliyeshika tama hajapata zawadi

       v.          Baba  analima  lakini kaka amesimama

(b) Chunguza jedwali lifuatalo kwa makini  kisha jaza sehemu zilizoachwa wazi

Neno

Mzizi

Kauli ya kutendana

Kauli ya kutendwa

Kusema

 

 

 

 

 

Kupigana

 

Kuomba

 

Kuombana

 

 

Andik­­­_

 

Kuandikwa

(c ) Tunga sentensi kwa kutumia vipashio vifuatavyo 

        i.          W+t+N 

      ii.          N+ V + Ts  +  T+ E

    iii.          W+Ts+Ts + T+E

     iv.          N+T+N

       v.          T

SEHEMU D : ALAMA (40 )

4. (a)   Kamilisha methali zifuatazo 

       i.          Kuishi kwingi…………………………..

     ii.          Mchuma janga …………………………….

   iii.          Chanda chema ……………………….

   iv.          Asiyekubali kushindwa ………………….

     v.          Jambo usilolijua ………………………..

(b) Eleza maana ya istilahi zifuatazo

       i.          Vina

     ii.          Hadhira

   iii.          Fani

   iv.          Mizani

     v.          Dhamira

 

(c  ) Fasihi simulizi hujitokeza katika tanzu kuu nne

Taja tanzu hizo na kwa kila tazu taja vipera viwili

TANZU

VIPERA

(i)

(i)

(ii)

(ii)

(iii)

(iii)

(iv)

(iv)

 

SEHEMU E (ALAMA 15)

UANDISHI WA INSHA /UTUNGAJI

5. Wewe ni mwanafunzi wa kidato cha pili katika shule ya sekondari Tegemeo ,s.L.P 130 Dodoma ,una matatizo ya kiafya ,hivyo unahitaji kwenda kutibiwa hospitali ya mkoa wa Dodoma .Adika barua kwa mkuu wako wa shule kuomba ruhusa ya siku mbili (02) jina lako liwe Juhudi Sabuni .

 

 

MWONGOZO WA USAHIHISHAJI

MTIHANI WA UTAMILIFU KIDATO CHA PILI 2021

SOMO LA KISWAHILI

 



www.onlineschoolbase.com

 
 

 

 

1.      Swali linamtaka mwanafunzi asome kifungu cha habari kisha ajibu  maswali aliyopewa

(a)  Dalali alitaka shilingi elfu sita na mia tano kama kianzio cha bei  ya Beberu (alama 02)

(b) Mzabuni wa kwanza alitaka kulipa shilingi elfu saba na mia mbili (alama 02)

( c) “Haya tena jamani sogeeni” Inamaana kuwa watu wa kusanyike eneo  ambalo mnada wa Beberu unaendelea ili wanunue (alama02)

(d) Maana ya maneno

                   i.          Dalali –mtu anayenadi na kuuza vitu vya mnada ,mnadi

                 ii.          Zabuni – uza kwa kushindania bei

               iii.          Nafuu – rahisi /nyepesi (alama 02@ 6)

                iv.          Kichwa cha habari hii ni  Mnada (alama 3)

SEHEMU B ALAMA 15

2.      UTUMIZI WA LUGHA NA USAHIHI WA MAANDISHI

(a)  (i) Inzi ameingia kwenye chai

(ii) Baba atakwenda safari kesho (Baba atasafiri kesho ) 

(iii) huwa namwambia lakini hanielewi

(iv) Ngo’mbe wangu wameibiwa

(v) Ninaumwa kifua daktari ,sijalala usiku  kucha (alama 1@= 05)

(b) (i) Watu wasingeweza kupashana habari

      (ii) Tusingeweza kutambua hisia

     (iii)Kusingekuwa  na utambulisho wa  jamii

    ( iv) Tusinge elimika (alama 1@= 05

 

C

Orodha A

i

ii

iii

iv

v

Orodha B

H

A

C

D

B

(ALAMA 1@= 05)

SEHEMU C (ALAM A 15 ) SARUFI

3.     (a) (i)    ana- t

(ii) Kwanza kushoto –V

(iii) Yake – V

(iv) Yule – W

(v) Lakini  - U (ALAMA 1@ = 05 )                

(b)               

NENO

MZIZI

KAULI YA KUTENDANA

KAULI YA KUTENDWA

Kusema

-sem-

Kusemana

Kusemwa

Kupiga

-pig-

Kupigana

Kupigwa

Kuomba

-omb-

Kuombana

Kuombwa

Kuandika

-Andik-

Kuandikana

Kuandikwa

ALAMA 1@= 05

 (C)  (i)  W+t+N- Mimi ni mwanafunzi

      (ii) N+    V+Ts +T+E-Mchezaji hodari  alikuwa anacheza uwanjani

      (iii) W+ Ts+Ts  +T+ E – Yeye alikuwa anataka kwenda sokoni

     (iv) N+T+N-Mwanafunzi anasoma kitabu

      (v) T- Anasoma            ( Alama 1@=  05)

 

SEHEMU D (ALAMA 40)   

4.     (a) (i) Kuishi kwingi ni kuona mengi

(ii) Mchuma janga hula na wakwao

(iii) chanda chema huvikwa pete

(iv) Asiyekubali kushindwa si mshindani

(v) Jambo usilolijua ni sawa na usiku wa giza

  (ALAMA 2@=      10) 

 

(b) (i) Vina  - silabi za kati na mwisho zenye kufanana katika kila mstari

   (ii) Hadhira – msikilizaji /mpokeaji wa kazi za fasihi

(iii) Fani- Umbo la nje la kazi ya fasihi 

(iv) Mizani – Ni idadi ya silabi zilizomo kwenye mstari wa shairi au tenzi

(v) Dhamira –Ni lengo la mtunzi wa kazi ya fasihi (ALAMA 3@= 15

(C  )

TANZU

VIPERA

(I) Hadithi

(i) Visasili

(ii) Soga

(ii) Ushairi

(i) Nyimbo

(ii) Mashairi

(iii) Semi

(i) Methali

(ii) nahau

(iv) Sanaa za maonesho

(i) Majigambo

(ii) Vichekesho

ALAMA 3@ =15

5.     Mtahiniwa anatakiwa kuzingatia muundo wa uandishi wa barua rasmi

-        Anuwani ya mwandikiwa (Shule ya sekondari Tegemeo, s.l.p 130 (alama 2 )

-        Dodoma  (Alama 01)

-        Tarehe (Alama 01)

-        Anuwani ya mwandishi (mkuu wa shule (alama 02 )

-        Mwanzo wa barua (alama  01)

-        Kichwa cha barua (alama  02)

-        Kiini cha barua (alama 02 )

-        Kimalizio cha barua (alama 01)

-        Sahihi na jina (alama 02 )

-        Cheo (alama 01 )

MFANO

Shule ya sekondari Tegemeo

s.l.p   130  

Dodoma

17/5/2021

Mkuu wa shule

Shule ya sekondari  Tegemeo                                                                                       

s.l.p 130 .

Dodoma

 

Ndg

 YAH : OMBI LA RUHUSA KWENDA KUTIBIWA HOSPITALI YA MKOA WA DODOMA

         Mimi ni mwanafunzi ninayesoma kidato cha pili

Ninaomba ninaomba ruhusa ya siku mbili kuanzia tarehe 17/5/2021 hadi tarehe 19/5/2021 ili niweze kwenda kutibiwa katika hospitali ya mkoa wa Dodoma .

Ninasumbuliwa na tatizo la kujaa gesi tumboni kwa muda sasa.

          Ni matumaini yangu kuwa ombi langu litakubaliwa

Natanguliza shukrani zangu za dhati

 

J.SABUNI

Juhudi Sabuni

( Kidato cha pili - A)

 

 

...
logoblog

Thanks for reading FORM TWO CHEMBA KISWAHILI MOCK EXAMINATIONS WITH ANSWERS | MTIHANI NA MAJIBU (MARKING SCHEME) YA MTIHANI WA MOCK KISWAHILI WILAYA YA CHEMBA

Previous
« Prev Post

No comments:

Post a Comment